Hebu nisikilizeni sasa niwaambie furaha yangu eeh
Najua kwamba sote ni ndugu na baba yetu mmoja'
Nawakumbuka waliodharauliwa hata kukosa dhamani
Mungu ndiye huinua hushusha mwamini atakuinua
Hata wale masikini, wale watoto wa mitaani
Najua maisha magumu kwenu ipo siku tutafika
Nawakumbuka wale waliochukiwa bure bila sababu
Wengine vita na mama wa kambo, manyanyaso kila siku
Kuna walo zaa tena, wakawatupa watoto
Kuna wasiojiweza chakula kwao ni shida
Kuna wanaotamani kutembea hawawezi
Walemavu na vipofu wakitamani kuponywa
Najua haya yote yapo sababu Mungu ndiye hupanga maisha
Katika maombi yangu nawakumbuka sana
Japo maisha ni shida, yasikutenge na Mungu
Endelea mwenzangu anajua nia yako
Ni mponyaji wa kweli ye ndo mgawa riziki
Kilio chako, hakika bwana anajua
Usichoke furaha yetu iko karibu
Katika maombi yangu nawakumbuka sana
Japo maisha ni shida, yasikutenge na Mungu
Endelea mwenzangu anajua nia yako
Ni mponyaji wa kweli ye ndo mgawa riziki
Kilio chako, hakika bwana anajua
Usichoke furaha yetu iko karibu
Nawakumbuka waliokataliwa duniani na wazazi eeh
Mama yako au baba mzazi wako alikukana aah
Najua dunia hii inachosha lakini usichoke ndugu
Ni baba wa wote wamchao Mungu ni mwaminifu eeh
Katika yeye nayaweza yote Mungu wangu hashindi eeh
Ni vyema nawakumbuka sasa tufurahi pamoja aah
Hata kama ni kifo kitutenge tutaishi pamoja eeh
Najua wengi wamepotea tena wawadhamini eeh
Ya nini uhuzunike mfariji wako yupo
Shida tunazopitia malipo yake uzima
Atawafuta machozi hautaona huzuni
Ajua makovu yako, majeraha ya dunia
Nawaombea wote msichoke ahadi yetu iko karibu
Katika maombi yangu nawakumbuka sana
Japo maisha ni shida, yasikutenge na Mungu
Endelea mwenzangu anajua nia yako
Ni mponyaji wa kweli ye ndo mgawa riziki
Kilio chako, hakika bwana anajua
Usichoke furaha yetu iko karibu
Katika maombi yangu nawakumbuka sana
Japo maisha ni shida, yasikutenge na Mungu
Endelea mwenzangu anajua nia yako
Ni mponyaji wa kweli ye ndo mgawa riziki
Kilio chako, hakika bwana anajua
Usichoke furaha yetu iko karibu
Nawakumbuka
Nawakumbuka Song Meaning, Biblical Reference and Inspiration
Japhet Zabron's song "Nawakumbuka," released on October 29, 2021, serves as a poignant reflection on the struggles faced by various marginalized and suffering groups in society. The title itself, meaning "I Remember Them," sets the tone for a song that is deeply empathetic and spiritually grounded. It begins by establishing a sense of shared humanity under one Father, setting the stage for an address that encompasses a wide range of human afflictions and social injustices. The song moves beyond a simple observation of suffering, positioning itself as an act of remembering these individuals in prayer and solidarity.
The lyrics paint a vivid picture of those who are often overlooked or mistreated. The artist explicitly mentions individuals who have been disregarded and undervalued, the poor, street children facing difficult lives, those hated without cause, victims of domestic abuse, children abandoned by their parents, those who are unable to provide for themselves, and the physically challenged including the disabled and the blind yearning for healing. This comprehensive list highlights the breadth of hardship present in the world and emphasizes the song's intent to bring these specific struggles to light.
Central to the song is the powerful affirmation of remembering these individuals "sana" (very much) in prayer. This repeated phrase underscores the spiritual core of the message, suggesting that active intercession is a vital response to witnessing such suffering. The artist encourages those struggling to remain connected with God despite their hardships, believing that God knows their intentions and their deepest cries. Prayer is presented not just as a personal act but as a means of collective support and remembrance for those in need.
The song weaves theological depth throughout its message, articulating a strong belief in God's sovereignty and His intimate involvement in human life. It states that God is the one who raises and lowers, implying His ultimate control and purpose even in difficult circumstances, as referenced in scriptures like 1 Samuel 2:8 and Psalm 113:7. Furthermore, the lyrics declare that God is the true healer and the provider of sustenance, echoing themes found in passages such as Philippians 4:19 and Isaiah 61:1. The recognition that God plans life ("Mungu ndiye hupanga maisha") aligns with biblical understanding of God's providence (Jeremiah 29:11), while the assurance that God knows one's intentions and suffering is a source of comfort, reflecting the omnipresence and compassion described in scriptures like Psalm 139 or Psalm 34:18.
Offering a message of unwavering hope and encouragement, "Nawakumbuka" urges listeners not to lose heart or become weary despite the trials they face. The song emphasizes that joy and the fulfillment of God's promises are near ("furaha yetu iko karibu," "ahadi yetu iko karibu"). It promises that God will wipe away tears and remove sorrow, a theme powerfully presented in Revelation 21:4. The assurance that the "payment" for current troubles is life ("malipo yake uzima") points towards eternal hope and the belief that through faith, all things are possible with God, as conveyed in Philippians 4:13. By acknowledging the "scars" and "wounds of the world," the song validates the pain experienced but swiftly redirects focus to the comforter who is present and active.
Ultimately, "Nawakumbuka" serves as a moving and inspirational anthem of faith, empathy, and perseverance. It is a call to remember those who are suffering, not just in thought but in active prayer and compassionate regard. The song provides a spiritual anchor for those facing hardship, reminding them of God's knowledge, power, and the promise of future relief and joy. It reinforces the belief that even in the darkest moments, faith in God offers solace and the strength to continue, knowing that a brighter future and the fulfillment of divine promises are within reach.